Sifa Kwa Bwana Lyrics – Light Bearers TZ Lyrics

Sifa Kwa Bwana Lyrics Light Bearers Tz

STANZA 1
Sauti yangu yaimba
sifa zako Bwana
kinywa changu chatangaza
wema wako Bwana
Katika siku zangu za kushi
nimeshuhudia mambo mengi sana
Mambo makuu sana uliyonitendea
Mambo makuu sana siwezi kueleza

PRE-CHORUS
Mkono wako ulinilinda
Nikiwa tumboni mwa mama
Siku yangu ya kuzaliwa ilipofika
nikawasili salama
E Bwana, Pokea sifa zangu

Watch Sifa Kwa Bwana Lyrics Video Here

CHORUS
Nina, Nina-Ipaza sauti yangu
Niki-Nikiimba Nikiimba
sifa zako Bwana
Wasta Wasta Wasta-hili kuabudiwa
Bwana jina lako liinuliwe juu X2

STANZA 2
Utotoni ulinilea na kunijali
Mabaya mengi
yaliniepusha Bwana wangu
Viganjani mwako ukanikuza
sasa tazama naleta wimbo kwako
Wimbo wa kusifu
lisifu jina lako
Wimbo wa kusifu
na kukwabudu wewe

PRE-CHORUS
Safari ndefu umenileta
nikumbukapo nilikotoka
Nisingekuwa nilivyo
isingekuwa wewe Bwana
acha nishukuru
Asante, asante Mungu wangu

FOLLOW OUR WHATSAPP CHANNEL FOR MORE UPDATES

CHORUS
Nina, Nina-Ipaza sauti yangu
Niki-Nikiimba Nikiimba
sifa zako Bwana
Wasta Wasta Wasta-hili kuabudiwa
Bwana jina lako liinuliwe juu X2

STANZA 3
Ipo siku nitaleta sifa kamili kwako
sifa zisizo kama za huku duniani
Maana sifa za huku duniani
zina kasoro nyingi nyingi sana
Siku nitatolewa hapa duniani
Siku nitasimama mbele zako Bwana

PRE-CHORUS
Sitakuwa na kinyongo tena
nitasimama kwa ujasiri
ulimi wangu na maneno yake yote
yatakuwa yametakasika
Ajabu nitaimba ajabu

CHORUS
Nina, Nina-Ipaza sauti yangu
Niki-Nikiimba Nikiimba
sifa zako Bwana
Wasta Wasta Wasta-hili kuabudiwa
Bwana jina lako liinuliwe juu X3

FOLLOW OUR WHATSAPP CHANNEL FOR MORE UPDATES

SHARE THIS POST