Pahali Pema Lyrics – Christ Followers Ministers Kisii

Pahali Pema Lyrics by Christ Followers Ministers

STANZA 1

Mtumishi wa Mungu Yoshua
akawaambia wanaisraeli basi mcheni Bwana
mkamtumikie kwa unyofu wa moyo
na kwa kweli mje hekaluni mwake kwa upole
yeye ni Baba yetu
hakuna mwingine tena
tokea mawio ya jua ametukuka milele
yeye ni Baba yetu
hakuna mwingine tena
tokea mawio ya jua ametukuka milele

Nanyi mkiona ni vibaya kumtumikia
Bwana Mungu
chagueni mtakayemtumikia
Andiko la Yoshua
mimi na nyumba yangu tutamtumikia
Mungu wa majeshi aishiye
hekaluni mwa Bwana ni kwa wenye subira
Aliyetutoa Misri akatupandisha juu
aliyezifanya ishara kubwa sana
mbele ya macho yetu
na kutulinda katika njia X2

Watch Pahali Pema Lyrics Video Here

CHORUS

Wanaoumia na kutekwa nyara
wasumbukao mioyo
waje kwake Bwana
wanaolemewa na mizigo mizito
wana majonzi tele
waje kwake Bwana
kwani (hapa ndipo pema
hapana pema tena
kwake Yesu ndipo penye pumziko la mioyo X2)

FOLLOW OUR WHATSAPP CHANNEL FOR MORE UPDATES

STANZA 2
Inua macho utazame mbinguni
ndipo penye tumaini la wanyonge
yeye ni Baba wetu hawezi tuacha
japo yawe machungu vumilia ndugu x2)

Huna wakati wa kupoteza dhambini
Yesu anaita leo
Bado kuna nafasi kwa anayetaka toba
Yesu anabisha mlango fungua
Kuna nchi nzuri sisi tumeahidiwa
baada ya dhiki mateso
Haijalishi vile sisi tumetanga mbali
ni mwingi wa rehema na neema X2

Watch Pahali Pema Official Video Here

CHORUS

Wanaoumia na kutekwa nyara
wasumbukao mioyo
waje kwake Bwana
wanaolemewa na mizigo mizito
wana majonzi tele
waje kwake Bwana
kwani (hapa ndipo pema
hapana pema tena
kwake Yesu ndipo penye pumziko la mioyo X2)

FOLLOW OUR WHATSAPP CHANNEL FOR MORE UPDATES

SHARE THIS POST